Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda

Baraza la Ushindani Halali wa Biashara

"Zinduka !!! Rufaa ni haki ya Mfanyabiashara na Mtumiaji wa Huduma na Bidhaa”

Kuhusu Sisi

Historia ya Baraza

Baraza la Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar (Zanzibar Fair Competition Tribunal – ZFCT) ni mojawapo ya Taasisi iliyoundwa chini ya kifungu cha 26 cha Sheria ya Ushindani Halali wa Biashara na kumlinda Mtumiaji Nambari 5 ya mwaka 2018.

Mwaka 1995, Serikali ilitunga sheria ya kufuta sheria ya kusimamia mwenendo wa biashara na kumlinda Mtumiaji ya Zanzibar Nam.2 ya mwaka 1995, na kutunga sheria mpya ya Ushindani Halali wa Biashara na kumlinda mtumiaji kuweka masharti bora zaidi pamoja na mambo mengine yanayohusiana na hayo. Baraza limeanza rasmi mnamo mwishoni mwa mwezi wa Oktoba 2020, baada ya kukamilika kwa uteuzi wa Mwenyekiti, Wajumbe na Mrajis wake.

DIRA

Kuwa Baraza bora la Rufaa katika masuala ya Ushindsni Halali wa Biashara.

DHAMIRA    

Kupokea na kutoa maamuzi ya mashauri ya Rufaa

Maadili ya Msingi ya Baraza

Baraza la Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar linafanya kazi kwa kufuata maadili ya msingi yafuatayo:

  1. Haki kwa wakati unaofaa
  2. Ufanisi na Tija
  3. Uadilifu na Heshima
  4. Usawa na Uhuru
  5. Ushirikiano
  6. Uwazi
Scroll to Top

example.com

example2.com

example3.com